KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 16, 2010

Pinto mwenyekiti mpya TASWA

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa), leo kimefanya uchaguzi wa viongozi watakaokaa madarakani kwa miaka mitatu katika uchaguzi uliofanyika ukumbi wa manispaa Kinondoni, Dar es Salaam. Mwenyekiti alichaguliwa Juma Pinto ambaye ni Mkurugenzi wa gazeti la JamboLeo,alipata kura 61 dhidi ya kura 11 za Mhariri wa gazeti la SpotiStarehe, Juma Pinto na kura nane za Mpoki Bukuku wa gazeti la Mwananchi. Mtangazaji wa Redio One, Maulid Kitenge aliibuka Makamu Mwenyekiti baada ya kupata kura 37 dhidi ya kura 31 za mtangazaji wa Clouds FM, Shafii Dauda na kura 11 za mtangazaji wa Star TV aliyekuwa akitetea wadhifa huo, Tom Chilala. Katibu Mkuu alichaguliwa Mhariri wa Michezo wa gazeti la HabariLeo, Amir Mhando aliyepata kura 78 za ndiyo, ambapo kura moja ilimkataa. Kura 79 zilipigwa na hakuwa na mpinzani, wakati Katibu Msaidizi ilienda kwa George John aliyepata kura 41 dhidi ya kura 38 za Nasongelya Kilyinga. Mhazini ilienda kwa Sultani Sikilo aliyepata kura 45 dhidi ya 32 za Dina Ismail, wakati Mhazini Msaidizi ni Mohammed Mkangara aliyepata kura 78 za ndiyo na moja ilimkataa. Wajumbe sita wa Kamati ya Utendaji walioshinda ni Zena Chande, Elius Kambili, Salum Jaba, Grace Hoka, Tulo Chambo na Onesmo Kapinga.

No comments:

Post a Comment