KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 18, 2010

Hellen Dausen kuwania taji la Miss Universe 2010 J'pili


MWAKILISHI wa Tanzania katika shindano la kumsaka ‘Miss Universe 2010’, Hellen Dausen mwishoni mwa wiki hii anatarajiwa kuwa mmoja wa warembo 83 kutoka sehemu mbalimbali duniani watakaowania taji hilo.
Hellen atapanda ulingoni na warembo wengine wanane kutoka Afrika, kuwania taji hilo kwenye shindano litakalofanyika kwenye ukumbi wa Mandalay Bay Events Center uliopo mjini Las Vegas.
Mshindi wa shindano hilo la 59 anatarajiwa kuvikwa taji la mrembo wa mwaka jana, Stefania Fernandez kutoka nchini Venezuela, ambaye alimvua taji Dayana Mendoza mwaka juzi.
Hellen anakuwa Mtanzania wa nne kuwania taji hilo tangu mwaka 2007 wakati mashindano hayo yalipoanzishwa hapa nchini na mwanadada Maria Sarungi.
Mtanzania wa kwanza kushiriki katika fainali hizo alikuwa Flaviana Matata mwaka 2007, ambaye alifanikiwa kuingia katika hatua ya 15 bora.
Alifuatiwa na Amanda Ole Sululu mwaka 2008 kabla ya Illuminata Mize mwaka jana. Washiriki hao wawili wote walitolewa hatua za awali.
Shindano la ‘Miss Universe’ ndilo kongwe kuliko mashindano yote ya urembo duniani. Lilianzishwa mwaka 1952.
Mbali na Hellen, warembo wengine kutoka Afrika wanaotarajiwa kuwania taji hilo ni Jurema Femaz wa Angola, Tirelo Ramasedi wa otswana, Domia Hammed wa Misri na Awurama Simpson wa Ghana.
Waafrika wengine wataopanda jukwaani kuwania taji hilo ni Dalysha Doorga wa Mauritius, Ngozi Odalonu wa Nigeria, Nicole Flint wa Afrika Kusini na Alice Musukwa wa Zambia.
Tayari washiriki wa shindano hilo wameshashindana katika hatua za awali, ambazo zilihusisha mavazi ya ufukweni na kuonyesha vipaji vyao katika michezo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment