KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, July 16, 2010

Nafurahia mwili wangu sasa-Janet Jackson


LOS ANGELES, Marekani
MWANAMUZIKI nyota wa zamani wa Marekani, Janet Jackson amesema, kwa sasa anaufuarhia zaidi mwili wake kuliko alivyokuwa miongo mitatu iliyopita.
Janet (44), mwanamuziki ndugu na waliokuwa wakiunda kundi la Jackson Five, alisema hayo kupitia jarida la Essence, toleo la hivi karibuni.
Akiwa na umri wa miaka 11 hadi 13, Janet alikuwa akishiriki kucheza vipindi vya televisheni vya Penny Woods na Good Times miaka ya 1970.
Lakini alidai alikuwa akijihisi vibaya kuhusu kukuwa kwa mwili wake wakati akishiriki kwenye vipindi mbalimbali vya televisheni ya Marekani.
“Wakati nikicheza kipindi cha Good Times, walinitaka nikibane kifua changu,”alisema.
“Nilianza kubadilika kimwili tangu nikiwa mdogo. Hawakunieleza iwapo wangenifanyia hivyo,”aliongeza.
Janet alisema wakati mwingine alikuwa akivalishwa masweta yanayobana kifua chake ili kukifanya kionekane hakina maziwa na kuongeza kuwa, hali hiyo ilikuwa ikimkera.
“Fikiria wewe ni mtoto usiye na hatia na mara unaanza kuwaza kwamba muonekano wako wa asili si mzuri. Hali hii iliniathiri sana,”alisema mwanamuziki huyo.
Janet, ambaye picha yake imetumika kwenye ukurasa wa mbele wa jarida la Essence toleo la hivi karibuni alisema kwa sasa amebadili mwelekeo.
Kwa sasa, mwanamuziki huyo anaandika kitabu kitakachoitwa True You, kinachozungumzia mazoezi ya mwili na vyakula vinavyofaa kuliwa.
“Nilitaka kuandika kitabu hiki kwa sababu nataka watoto wapate kitu cha kusoka na kuelewa kwamba wao ni wazuri kwa jinsi walivyo,”alisema.
“Ilinichukua muda kuwa hivi nilivyo sasa. Lakini napenda maisha yangu. Natamani ningekuwa na msimamo huu tangu nikiwa mdogo. Lakini siku zote kila kitu hutokea kwa sababu maalumu,”aliongeza.
Licha ya kifo cha kaka yake, Michael Jackson mwaka jana, Janet alisema anayafurahia maisha yake.
“Nina bahati. Kwa sasa nipo huru,”alisema mwanamuziki huyo, aliyetengana na mchumba wake wa miaka mingi, Jermeine Dupri mwaka 2009.
“Siwezi tena kuingizwa kwenye mtego wa mkataba ambao siufurahii. Nipo huru na nafurahia hali hii. Naweza kufanya chochote ninachokitaka,”alisema.
Hivi karibuni, Janet alikutwa akivinjari na Wissam Al Mana, mwanaume anayedaiwa kuwa na umri mkubwa kuliko yeye, akiwa amemzidi kwa miaka kumi.

No comments:

Post a Comment