KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 11, 2010

HISPANIA BINGWA WA DUNIA





HISPANIA jana ilitwaa ubingwa wa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya kuichapa Uholanzi bao 1-0 katika mechi ya fainali iliyochezwa kwenye uwanja wa Soccer City mjini Johannesburg.

Bao pekee na la ushindi la Hispania lilipachikwa wavuni na kiungo Andres Iniesta katika muda wa nyongeza wa dakika 30 baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 zikiwa suluhu.

Iniesta alifunga bao hilo dakika ya 116 baada ya kupokea pasi maridhawa kutoka kwa Cesc Fabregas na kufumua shuti lililompita kipa Maarten Stekelenburg wa Uholanzi.

No comments:

Post a Comment