KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, July 16, 2010

MAMBO YA SIKINDE

MPIGA gita la besi wa Mlimani Park Orchestra, Charles John Ngosha akifanya vitu vyake wakati wa onyesho hilo.
MHARIRI wa gazeti la Burudani, Rashid Zahor akimkabidhi zawadi ya fulana shabiki wa Sikinde, Shabani Jiwe kutokana na kutokosekana kwenye maonyesho ya bendi hiyo yanayofanyika kila siku za Jumapili kwenye ukumbi wa DDC Kariakoo, Dar es Salaam.

MWIMBAJI nyota na mkongwe wa Mlimani Park Orchestra, Hassan Bitchuka akiimba moja ya vibao vya zamani vya bendi hiyo wakati wa onyesho hilo.



WAPULIZA trumphet wa bendi ya Mlimani Park, Mbaraka Othman (kushoto) na Hamisi Milambo wakifanya vitu vyao wakati wa onyesho la juzi.



MHARIRI wa gazeti la Burudani, Rashid Zahor (kulia) akizunguma na wanamuziki pamoja na
mashabiki wa bendi ya Mlimani Park Orchestra wakati wa onyesho lililofanyika juzi kwenye ukumbi wa DDC Kariakoo, Dar es Salaam. Kushoto ni msemaji mkuu wa bendi hiyo, Jimmy Chika na katikati na mwanamuziki Hassan Kunyata. (Picha zote na Emmanuel Ndege).




WAIMBAJI wa bendi ya Mlimani Park Orchestra wakiwajibika jukwaani wakati wa onyesho hilo. Kutoka kushoto ni Hassan Kunyata, Abdalla Hemba na Shaabani Dede.
















No comments:

Post a Comment