KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, July 8, 2010

Mrembo wa Temeke kusakwa kesho




WAREMBO 14 kesho wanatarajiwa kupanda jukwaani kuwania taji la mrembo wa Kanda ya Temeke 2010 katika shindano litakalofanyika kwenye ukumbi wa klabu ya Sigara, Chang’ombe, Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kampuni ya BMP Promotions, Benny Kisaka alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, warembo hao wanatoka katika vitongoji vya Kurasini na Chang’ombe.
Benny alisema ana hakika mshindi wa kanda hiyo ndiye atakayenyakua taji la mrembo wa Tanzania mwaka huu, baada ya kulikosa taji hilo kwa miaka miwili.
Kwa mujibu wa Benny, karibu washiriki wote wa shindano hilo wana sifa na vigezo vinavyotakiwa, hivyo alitabiri kuwa ushindani utakuwa mgumu.
Benny alisema kamati ya Miss Temeke ilikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa, wanapatikana warembo bomba kwa ajili ya kuwania taji hilo mwaka huu ili mshindi afanye vizuri katika shindano la Miss Tanzania.
Kabla ya kuanza kwa shindano hilo, Benny alisema washiriki watafanya onyesho maalumu la muziki walilofundishwa na Caroline Zayumba na Dickson Guntram kutoka kundi la THT.
Benny alisema shindano hilo litapambwa kwa burudani mbalimbali za muziki kutoka kwa wasanii Banana Zorro na baba yake, Zahir Ally Zorro pamoja na wacheza shoo wa bendi ya Twanga Pepeta International.
Taji la Miss Temeke kwa sasa linashikiliwa na Sia Ndaskoy.

No comments:

Post a Comment