KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 17, 2017

YANGA BINGWA


BAO lililofungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amis Tambwe, jana liliiwezesha Yanga kuichapa Toto African bao 1-0 na kutwaa tena taji la ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku ikiwa na ushindani mkali, Yanga ilipata bao hilo la pekee dakika ya 72 baada ya Tambwe kujitwisha kwa kichwa krosi kutoka kwa beki Juma Abdul.

Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa Yanga kutwaa taji hilo, safari hii ikiwa chini ya Kocha George Lwandamina kutoka Zambia. Awali, Yanga ilitwaa taji hilo mara mbili ikiwa chini ya Hans Van Der Puijm.

Kipigo hicho kimeiweka Toto African kwenye hatari ya kushuka daraja msimu ujao huku ikiwa imesaliwa na mechi moja dhidi ya Mtibwa Sugar, itakayochezwa kwenye uwanja wa Manungu, ulioko Turiani, Morogoro.

Kwa upande wa Yanga, ushindi huo umeiwezesha kuwa na pointi 68, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 65 huku kila timu ikiwa imesaliwa na mechi moja kumaliza ligi.

Simba itamaliza ligi kwa kuvaana na Mwadui kwenye Uwanja wa Taifa wakati Yanga itavaana na Mbao FC kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba itaweza kutwaa ubingwa iwapo itaifunga Mwadui mabao 10-0 na wakati huo huo Yanga kufungwa na Mbao.

No comments:

Post a Comment