KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 23, 2017

SPORTPESA YAMWAGA MAMILIONI SINGIDA UNITED




Kampuni ya michezo ya kubashiri ya SportPesa imeendelea kuonesha dhamira yake katika kuhakikisha Ligi Kuu soka Tanzania bara msimu ujao 2017/2018 kunakuwa na ushindani wa kweli kutoka katika timu mbalimbli kutokana na jitihada zake za kudhamini vilabu kadhaa.

Baada ya kuingia mkataba wa udhamini na Simba na Yanga katika kipindi cha miaka mitano wenye thamani ya zaidi ya Tsh Bilioni 4, leo May 23 wametangaza kuingia mkataba wa mwaka mmoja wa udhamini na club ya Singida United ya Singida wenye thamani ya Tsh milioni 250.

SportPesa kuonesha kuwa wanajali kuinua vipaji na kulenga kuinua soka la Bongo wameidhamini Singida United licha ya kuwa ndio imepanda Ligi Kuu Tanzania bara msimu huu na itashiriki Ligi Kuu msimu ujao wa 2017/2018.

No comments:

Post a Comment