KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 30, 2017

SIMBA YATWAA KOMBE LA FA


SIMBA imefanikiwa kutwaa Kombe la Shirikisho la Azam baada ya kuibwaga Mbao FC mabao 2-1 katika mechi ya fainali iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Mshindi wa pambano hilo ilibidi apatikane katika muda wa nyongeza wa dakika 30, baada ya timu hizo kumaliza dakika 90 zikiwa suluhu.

Simba ilikuwa ya kwanza kupata bao katika muda huo wa nyongeza lililofungwa na Frederick Blagnon kabla ya Mbao FC kusawazisha kupitia kwa Robert Ndaki.

Zikiwa zimesalia dakika chache za muda wa nyongeza kumalizika, Simba ilipata bao la pili lililofungwa kwa njia ya penalti na Shiza Kichuya baada ya beki mmoja wa Mbao kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment