KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, May 15, 2017

MSHAMBULIAJI WA MAMELOD SUNDOWNS ATUA SINGIDA UNITED


Singida United imedhamiria kuleta mapinduzi ya soka hapa nchini baada ya klabu hiyo kuendelea kujiimarisha zaidi kwenye usajili wa wachezaji.

Baada ya kufanikiwa kusajili wachezaji wanne wa kigeni leo hii uongozi wa klabu hiyo umekamilisha usajili wa mshambuliaji aliyewai kuitumikia ya Mamelod Sondowns na Super Sport za nchini Afrika ya Kusini.

Mshambuliaji huyo anaetambulika kwa jina la Nhivi Simbarashe anakuwa mchezaji wa tano kusajili ndani ya klabu hiyo itakayoongozwa na kocha mahili Hans van Der Pluijm na msaidizi wake Fredrick Minziro.

Simbarashe pia ni mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Zimbabwe amekuwa na mafanikio makubwa kwenye timu alizochezea ikiwemo kufunga goli pekee ambalo liliwaondosha TP Mazembe katika ushiriki wa michuano ya kombe la klabu bingwa barani Afrika wakati akiitumikia timu ya Mamelod Sondowns.

Uongozi wa Singida United umethibitisha kumpa kandarasi ya miaka miwili mchezaji huyo akitokea klabu ya Caps United ya nchini Zimbabwe ambapo baada ya kutokea Afrika Kusini alijiunga na timu hiyo ya nchini kwake.

No comments:

Post a Comment