KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 12, 2017

MAN UNITED, AJAX SASA KUVAANA FAINALI YA KOMBE LA UROPA



Manchester United wameshashinda kombe la Champions League, klabu bingwa dunia, FA na makombe mengine lakini hawajawahi kishinda kombe la Europa.

United wamepata nafasi kujaribu kushinda kombe hilo kwa mara ya kwanza baada ya hapo jana kutoka suluhu ya bao moja kwa moja dhidi ya Celta Vigo ya nchini Hispania.

Katika mchezo huo timu zote zilimaliza pungufu uwanjani baada ya Eric Bailly kwa upande wa United na Rocanglia wa Celta Vigo kuoneshwa kadi nyekundu ikiwa imebaki dakika moja kwa mchezo kumalizika.

United walianza kupata bao dakika ya 17 baada ya Fellaini kuunganisha kwa kichwa mpira wa Marcus Rashford na bao hilo kuifanya United kwa mara ya kwanza kufunga mabao 100 katika msimu mmoja tangu mwaka 2012/2013.

Dakika zikiwa ximebaki 5 kufikia dakika ya 90 Celta Vigo walisawazisha bao hilo kupitia kwa Sebastian Rocanglia ambaye dakika 4 baadae alipewa kadi nyekundu.suluhu imewafanya United kufudhu kucheza fainali kwa jumla ya mabao 2 kwa 1 kutokana na ushindi wao wa kwanza walioupata ugenini wiki iliyopita.

Fainali hii ni ya 14 kwa kocha wa United Jose katika mashindano yote toka aanze ukocha lakini rekodi yake ikiwa nzuri kwani katika fainali 13 alizowahi kufika, ameshindwa fainali 2 tu kubeba ubingwa.

Huko Ufaransa almanusra Olympique Lyon wabadili matokeo ya mwanzo ambapo walifungwa bao 4 kwa 1 na Ajax mjini Amsterdam na hapo jana wakiwa nyumbani walibakiza bao 1 tu kuweka mambo sawa.

Ushindi wao wa bao 3 kwa 1 haukutosha kuwasogeza katika fainali lakini shukrani kwa Alexandre Lacazatte ambaye alifunga mara mbili kwa Lyon na lile la tatu likifungwa na Rachid Ghezzal huku la Ajax likifungwa na Kasper Dolberg.

Tarehe 24 mwezi huu ndio ambapo bingwa wa Europa atafahamika ambapo United na Ajax watakutana katika dimba la Friends Arena lililoko Stochklom nchini Sweden.

No comments:

Post a Comment