KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 16, 2017

SERENGETI BOYS YAWATOA NISHAI MABINGWA WATETEZI MALI


LIBREVILLE, Gabon

TIMU ya soka ya Taifa ya Vijana wa chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, jana walianza vyema michuano ya fainali za kuwania ubingwa wa Afrika baada ya kuwalazimisha kutoka suluhu mabingwa watetezi Mali.

Katika mechi hiyo ya kundi B iliyochezwa mjini hapa, Mali ilicheza vizuri kipindi cha kwanza na kulitia msukosuko mara kwa mara lango la Serengeti Boys, lakini haikuwa na bahati ya kupata bao.

Katika kipindi hicho, Serengeti Boys ilipwaya kutokana na safu yake ya kiungo kuzidiwa na wapinzani wao. Hadi kilipomalizika, hakuna timu iliyoweza kupata bao.

Kocha Bakari Shime alifanya mabadiliko mawili ya wachezaji kipindi cha pili, ambayo yaliongeza uhai kwa Serengeti Boys, iliyowapa kazi ya ziada mabeki wa Mali kuokoa mipira ya hatari na kupunguza nguvu yao ya kushambulia.

Katika kipindi hicho, Serengeti Boys ilifika kwenye lango la Mali zaidi ya mara tatu, lakini mashuti ya washambuliaji wake Nashon, Yohanna Mkomola na Nickson Kibambage yalishindwa kulenga lango.

Kipa Ramadhani Kambwili aliiokoa Serengeti Boys iisifungwe dakika ya 77 baada ya kuzuia kwa mguu shuti la Lassan Traole, lililokuwa likielekea wavuni na mpira kuwa kona.

Serengeti Boys imesaliwa na mechi mbili dhidi ya Niger na Angola na iwapo itashinda zote, itafuzu kucheza nusu fainali na kupata tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini India.

No comments:

Post a Comment