KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 10, 2017

LIGI KUU YA VODACOM BARA KUENDELEA KESHO, SIMBA KUVAANA NA STAND UNITED


Mara baada ya michezo ya mwishoni mwa juma lililopita, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2016/2017, inatarajiwa kuendelea Ijumaa Mei 12, 2017 ambako Simba SC itaialika Stand United FC ya Shinyanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Azam FC siku hiyo hiyo ya Mei 12, mwaka huu itakuwa mwenyeji wa Toto Africans ya Mwanza kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam.

Jumamosi Mei 13, mwaka huu JKT Ruvu itakuwa nyumbani Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kucheza na Majimaji ya Songea wakati Tanzania Prisons itaikaribisha Ndanda ya Mtwara kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya ilihali Mwadui ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Manungu ulioko Mvomero, Morogoro huku Mbeya City ikisafiri hadi Dar es Salaam kucheza na Young Africans kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Siku ya Jumapili Mei 14, mwaka huu African Lyon ya Dar es Salaam itacheza na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam ilihali siku inayofuata, Jumanne Mei 16, mwaka huu Young Africans tena itakuwa mwenyeji wa Toto Africans kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Funga dimba la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara itakuwa Mei 20, mwaka huu kwa timu zote kucheza ambako Azam FC itakuwa mwenyeji wa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Majimaji itamaliza na Mbeya City kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea wakati Simba na Mwadui zitacheza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Siku hiyo Mbao FC itaialika Young Africans ya Dar es Salaam kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza wakati Stand United itamaliza na Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja Kambarage mjini Shinyanga ilihali Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa Toto Africans ya Mwanza kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro wakati Africans Lyon ikiwa mgeni wa Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na Ndanda itamaliza na JKT Ruvu mjini Mtwara kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona.

No comments:

Post a Comment