KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 11, 2017

BLOGU YA LIWAZOZITO YATIMIZA MIAKA SABA, YAFIKISHA WASOMAJI ZAIDI YA MILIONI MOJA


Kwa heshima na taadhima napenda kuwajulisha wasomaji wangu wa blogu ya liwazozito kwamba, blogu yenu pendwa, ambayo ni mahsusi kwa ajili ya habari za michezo na burudani, kesho inatimiza miaka saba tangu ilipoanzishwa mwaka 2010.

Blogu hii ilianza kwa mwendo wa kusuasua kutokana na ugeni wa teknolojia ya mitandao ya kijamii, lakini hatimaye ikaanza kukaza mwendo na sasa inakwenda kwa spidi kali, huku ikiendelea kuwapa habari motomoto zinazohusu michezo na burudani za aina mbalimbali.

Hadi sasa blogu hii imeshafikisha wasomaji 1,003,410 (takwimu za leo-Mei 11,2017), huku ikisomwa na watu wa mataifa mbalimbali barani Afrika, Ulaya, Arabuni na Marekani.

Nawashukuru sana wasomaji wangu wa hapa nchini, ambao wamekuwa wakinipa maoni na mawazo mbalimbali ya jinsi ya kuiboresha.

Wakati mwingine nilijikuta nikipigiwa simu usiku wa manane au alfajiri. Nikipokea, nakutana na maswali ya wasomaji wangu wanaotaka kujulishwa kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu ligi kuu ya Tanzania Bara, Ligi Kuu ya England, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na klabu za Simba na Yanga.

Mwanzoni nilikuwa naona kero, lakini baada ya muda si mrefu nikaanza kuzoea hali hiyo na kuwapa majibu kadri nilivyoweza. Ilikuwa changamoto nzuri, lakini iliweza kunijulisha ni kwa kiasi gani blogu hii inasomwa na watu wengi, hasa ikizingatiwa kuwa wapigaji walikuwa wanatoka katika mikoa karibu yote nchini.

Mafanikio ya blogu hii kihabari (sio matangazo), ndio yaliyoniwezesha kuanzisha blogu nyingine maalumu ya muziki wa taarab, maarufu kwa jina la ramozaone.blogspot.com (rusharoho) na nyingine kuhusu habari za kisiasa, biashara, uchumi na kijamii, inayoitwa tanzaniakwanzadaima.blogspot.com.

Asanteni sana wasomaji wangu kwa kuniunga mkono. Nawapenda sana.

No comments:

Post a Comment