KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 25, 2017

WACHEZAJI SERENGETI BOYS SASA WAHAMISHIWA KIKOSI CHA NGORONGORO HEROES




Rais wa TFF, Jamal Malinzi amesema kikosi cha timu ya taifa ya vijana wa chini ya umri wa miaka 17, Serengeto Biys, sasa watnaunda kikosi kipya cha taifa cha vijana wenye umri wa chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes.

Amesema kauli mbiu ya Ngorongoro Heroes, ni kanyaga twende mpaka kufuzu fainali za AFCON u 20 mwaka 2019, ambapo michezo ya kufuzu kwa hatua hiyo ya fainali za U-20 zitaanza Aprili, mwakani.

Alisema vijana hao wataingia kambini  Oktoba, mwaka huu na watacheza mechi ya kimataifa ya kujipima nguvu.

“Mpira huwa haulali, unachezwa saa 24 katika wiki duniani ambako huanzia Januari hadi Desemba, likimalizika shindano hili linakuja jingine. Maumivu ya kufungwa huwa ni mafupi, mashabiki siku zote huwa wanafkiria mechi ijayo. Tujiandae na Qulifiers za 2019 AFCON u-20, haziko mbali,” amesema.

Timu hiyo ya vijana ilikuwa jijini Libreville nchini Gabon kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika ya vijana iliyofanyika katika miji miwili ya Libreville na Port Gentil ambako iliondolewa kwenye hatua ya makundi na Niger.

Serengeti Boys ilifungwa bao 1-0 na Niger katika mchezo uliofanyika Port Gentil, hivyo kufanya matokeo ya timu zote mbili yaani Niger na Tanzania kufanana kwa pointi, idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa tangu kuanza kwa fainali hizi za AFCON, Mei 15, mwaka huu.

Serengeti Boys iliyokuwa Kundi B iliondolewa Kundi B iliondolewa na Niger iliyopenya kwenda hatua ya Nusu Fainali kwa faida ya kupata ushindi katika mchezo ambao umekutanisha timu hizo kwani Tanzania ilifungwa 1-0 katika mchezo wa mwisho hatua ya makundi. 

Kanuni hiyo ya mashindano ya CAF inajieleza kuwa matokeo ya ‘head to head’ kwa maana zinapokutana timu mbili zenye uwiano wa pointi na magoli matokeo huamualiwa kwa mshindi kupewa nafsi katika mchezo uliokutanisha timu hizo mbili.

No comments:

Post a Comment