KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, November 2, 2015

TWIGA STARS YAENDELEA KUWANOLEA KICHINJIO MALAWI




Timu ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ inayonolewa na kocha mkuu Rogasian Kaijage imendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Timu ya Taifa ya Wanawake ya Malawi utakaochezwa Novemba 07, mwaka huu jijini Dar es salaam katika uwanja wa Azam Chamazi.

Twiga Stars iliingia kambini Oktoba 29, katika hosteli za Shirikisho zilizopo Karume, ina kikosi cha wachezaji 22 wanaofanya mazoezi asubuhi na jioni katika uwanja wa Karume.

Mchezo dhidi ya Malawi ni mchezo wa kirafiki wa kimataifa, ambao kocha Kaijage atautumia kuangalia maendeleo ya wachezaji wake kwa ajili ya maandalizi ya micheo ya kimataifa.

Wachezaji waliopo kambini ni Asha Rashid, Estha Chaburuma, Fatuma Bushiri, Fatuma Omari, Mwajuma Abdallah, Mwanahamis Omar, Fatuma Khatibu, Amina Ally, Fatuma Issa, Belina Julius, Happines Hezron na Donizia Daniel.

Wengine ni Maimuma Hamisi, Stumai Abdallah, Anna Hebron, Anastazia Anthony, Shelder Boniface, Wema Richard, Tumaini Michael, Jane Cloudy, Saada Ramadhani na Sofia Mwasikili.

No comments:

Post a Comment