KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 11, 2015

KILIMANJARO STARS YAPANGWA KUNDI MOJA NA ETHIOPIA KOMBE LA CHALENJI




Ratiba ya michuano ya Kombe la Challenji kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa Senior Challenger Cup) imetoka jana ambapo timu ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Star’ imepangwa kundi moja na wenyeji Ethiopia.

Katika taarifa ya CECAFA iliyotolewa jana, Kilimanjaro Star imepangwa kundi A pamoja na wenyeji Ethiopia, Somalia na waalikwa wa michuano hiyo timu ya Taifa ya Zambia ‘Chipolopolo’.

Kundi B lina  Bingwa mtetezi timu ya Kenya, Uganda, Burundi na Djibouti, huku kundi C likiwa na timu za Rwanda, Sudan, Sudan Kusini na Zanzibar.

Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Novemba 21 nchini Ethiopia katika mji wa Addis Ababa na kumalizika Disemba 6 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment