KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 11, 2015

KIBADENI KOCHA MKUU KILIMANJARO STARS


Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limemteua Abdallah Kibadeni kuwa kocha mkuu wa timu wa Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Star’ akisaidiwa na Juma Mgunda kuelekea katika michuano ya CECAFA Chelenji itakayoanza kutimua vumbi Novemba 21 mjii Addis Ababa, Ethiopia.

Kilimanjaro Stars inashiriki michuano hiyo mikongwe kabisa barani Afrika, ambapo jumla ya nchi 12 wanachama wamedhibitisha kushiriki michuano hiyo itakayomalizika Disemba 6 mwaka huu.

Nchi zingine zinazoshiriki michuano hiyo ni tofati na Tanzania bara ni Burundi, Djibouti, Ethiopia, Eritrea, Kenya, Rwanda, Somalia, Sudani, Sudani Kusini, Uganda na Zanzibar.

Kibadeni mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, na timu ya Taifa Tanzania, ni kocha mwenye leseni B, ambapo ameshafundisha klabu nyingi nchini kwa mafanikio ikiwemo kuifikisha Simba katika hatua ya fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993.

Kocha Kibadeni ni mkurugenzi wa ufundi wa kituo cha mchezo cha KISA kilichopo Chanika, amewahi pia kuzifundisha timu za Kagera Sugar, JKT Ruvu.

Kocha msaidizi wa Kilimanjaro Stars, Juma Mgunda ana leseni B ya CAF, zamani alikuwa mshambuliaji wa timu ya Coastal Union na timu ya Taifa Tanzania, pia aliweza cheza soka la kulipwa katika klabu ya Nahd nchini Oman.

Mgunda amewahi kuifundisha timu ya Coastal Union ya jijini Tanga, timu ya mkoa wa Tanga, kocha wa kituo cha vijana cha mkoa wa Tanga.

Aidha Mgunda ni mkufunzi wa msaidizi wa mafunzo ya makocha ngazi pevu.

No comments:

Post a Comment