KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 24, 2010

TMK Wanaume Family: Hakuna mchezo



KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family lipo mbioni kuachia singo ya ‘Hakuna mchezo’, ambayo ni sehemu ya maandalizi ya albamu yao ya tatu.

Kiongozi wa kundi hilo, Rashid Ziada 'KR' alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, wimbo huo unatarajiwa kuanza kuchezwa mwezi ujao katika vituo mbalimbali vya radio nchini.

KR alisema kwa sasa wapo katika hatua za mwisho za kukamilisha kazi ya kurekodi singo hiyo, ambayo aliielezea kuwa, itakuwa moto wa kuotea mbali.

Alisema kundi lao lilikuwa kimya kwa muda ili kutoa nafasi kwa baadhi ya wasanii kutoa kazi zao katika mtindo huru (solo artist), ambapo baada ya kupita katika hatua hiyo, wanajiandaa kutayarisha albamu yao.

KR (33) alisema walimpisha Mheshimiwa Temba na Chege Chigunda kutoa nyimbo zao mpya na baada ya kukamilisha, imefika zamu ya kundi hilo kuendelea kupika nyimbo mpya.

TMK hadi sasa imetoa albamu mbili ambazo ni ‘Kazi ipo’ na ‘Ndio zetu'.

Katika hatua nyingine, KR amesema Aprili mwakani atazindua albamu yake nje ya kundi hilo. Amesema albamu hiyo itakuwa na nyimbo 10 na mpaka sasa ameshakamilisha nyimbo saba.

No comments:

Post a Comment