KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 24, 2010

Dk. Nchimbi kuongoza michezo



RAIS Jakaya Kikwete amemteua Dk. Emmanuel Nchimbi kuwa Waziri wa Habari, Vijana na Michezo.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Nchimbi alikuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa katika awamu ya kwanza ya serikali ya nne ya Rais Kikwete.

Dk. Nchimbi amechukua nafasi ya George Mkuchika, ambaye katika baraza jipya lililotangazwa jana, amehamishiwa katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Katika uteuzi huo, Rais Kikwete pia amemteua Dk. Renella Mukangara kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana na Michezo.

Dk. Renella amechukua nafasi ya Joel Bendera, ambaye alishindwa katika kura za maoni za uteuzi wa mbunge wa jimbo la Korogwe Vijijini.

No comments:

Post a Comment