KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 17, 2010

'Banana hakuwahi kunikataza kujihusisha na muziki'


MSANII nyota wa kike wa muziki wa kizazi kipya nchini, Maunda Zorro amesema kamwe kaka yake, Banana Zorro hakuwahi kumkataza kujihusisha muziki katika maisha yake.
Badala yake, Maunda amesema alichokuwa akikifanya Banana ni kumuusia mara kwa mara kumaliza kwanza masomo yake kabla ya kujitosa kwenye muziki.
Akihojiwa katika kipindi cha Burudani ni Nyumbani cha TBC 1 mwishoni mwa wiki iliyopita, Maunda alisema Banana alimpa usia huo kwa sababu fani hiyo ilimuathiri kwa kumfanya ashindwe kuyapa kipaumbele masomo yake.
"Ukweli ni kwamba Banana hakuwahi kunikataza mimi nisijihusishe na muziki. Alichokuwa akiniusia ni kuweka mbele masomo kwanza kabla ya kujitosa kwenye muziki,"alisema.
"Alikuwa akiniambia, hakuna kwenda studio wala kurekodi wimbo, nitafanya hivyo baada ya kumaliza masomo,"aliongeza.
"Banana alifanya hivyo kwa sababu alishabaini tatizo la kuchanganya muziki na masomo kwa vile lilimkuta. Alipokuwa akisoma sekondari, muziki ulimuingia sana kwenye damu yake kiasi kwamba alishindwa kuyapa kipaumbele masomo. Hakutaka nami niingie kwenye mkumbo huo,"alisisitiza.
Kwa mujibu wa Maunda, kwa sasa Banana amekuwa mstari wa mbele kumpatia misaada ya aina mbalimbali kimuziki ili aweze kufanikisha ndoto yake ya kuwa mwanamuziki.

No comments:

Post a Comment