KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 3, 2014

SIMBA YAIGAGADUA JKT OLJORO



SIMBA imefufua matumaini ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa JKT Oljoro katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo, mshambuliaji Hamisi Tambwe aliweka rekodi ya kuifungia tena Simba mabao matatu katika mechi moja na kuzawadiwa mpira. Bao lingine lilifungwa na kiungo Jonas Mkude.

Matokeo hayo yaliiwezesha Simba kuwa na pointi 30 baada ya kucheza mechi 15, ikiwa nafasi ya nne nyuma ya Mbeya City yenye pointi 31, Yanga yenye pointi 32 na Azam yenye pointi 33.

Mshambuliaji machachari wa Simba, Ramadhani Singano 'Messi' aliendelea kudhihirisha makali yake baada ya kutoa pasi nne maridhawa zilizozaa mabao hayo manne.

Kikosi cha Simba SC leo kilikuwa; Ivo Mapunda, William Lucian ‘Gallas’, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Donald Mosoti, Joseph Owino, Jonas Mkude, Haroun Chanongo, Awadh Juma, Amri Kiemba/Uhuru Suleiman dk64, Amisi Tambwe/Abdulhalim Humud na Ramadhani Singano ‘Messi’/Said Ndemla dk55.

JKT Oljoro; Mohamed Ali, Paul Malipesa, Ali, Omar, Nurdin Mohamed, Sabri Makame, Babu Ally, Jacob Masawe, Amir Omar, Shijja Mkina na Majaliwa Mbaga/Shaibu Nayopa dk38

No comments:

Post a Comment