KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, February 28, 2014

SIMBA KUTUMIA MIL 100/- KUJENGA UWANJA BUNJU




NA AMINA ATHUMANI
KLABU ya Simba imetangaza kujenga uwanja wake ndani ya siku 100 na kuanza kuutumia kwa ajili ya mazoezi ya timu hiyo.

Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, uwanja huo ambao utawekewa nyasi bandia, utaanza kufanyiwa maandalizi ya ujenzi kuanzia mwishoni mwa wiki hii.

Kamwaga alisema katika maandalizi ya ujenzi wa uwanja huo, wanachama wa klabu hiyo wanaombwa kujitokeza kwa wingi Jumamosi kwenda kufanya usafi kwa ajili ya maaandalizi ya ujenzi huo.

"Klabu sasa imeamua kwa nguvu zote kuanza ujenzi wa uwanja wake, na maandalizi kwa ajili ya ujenzi huo yaatanza Jumamosi," alisema Kamwaga.

Katibu huyo alisema maandalizi mengine kwa ajili ya ujenzi huo yanaendelea vizuri ikiwa ni pamoja na kukamilisha taratibu na kampuni itakayosimamia ujenzi huo.

Alisema kwa sasa klabu yake itajenga sehemu ya uwanja wa kuchezea soka kabla ya kujenga sehemu ya pili ya majukwa na kuwekwa maduka na hosteli za wachezaji.

Alisema ni matarajio yake kuwa uwanja huo utakamilika ndani ya siku hizo kama ilivyopangwa na kuanza kutumika mara moja ikiwa ni pamoja na kufanya maandalizi ya msimu ujao wa ligi.

No comments:

Post a Comment