KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, February 28, 2014

UKWA ASHEREHEKEA KUTIMIZA MIAKA 34




LAGOS, Nigeria
MMOJA wa wacheza filamu nyota wa Nigeria, Osita Iheme, maarufu zaidi kwa majina ya Pawpaw na Ukwa, mwishoni mwa wiki iliyopita alisherehekea kutimiza umri wa miaka 34.

Ukwa aliandaa sherehe hiyo kiasili, kijijini kwake Obeagu, Mashariki mwa Nkanu katika Jimbo la Nigeria.

Mshindi huyo wa tuzo mbalimbali za filamu nchini Nigeria, alisherehekea siku hiyo akiwa na rafiki zake, wacheza filamu wenzake na mashabiki wake wanaoishi Obeagu.

Kwa sasa, Ukwa yuko katika maandalizi ya kucheza filamu mpya, akiwa na swahiba wake mkubwa, Chinedu Ikedieze, maarufu kwa jina la Aki na waigizaji wengine.

"Naona fahari na heshima kuwa na watu hawa na pia nimeridhishwa na zawadi ndogo nilizopewa na waigizaji wenzangu hapa kwa ajili ya kusherehekea siku hii,"alisema Ukwa wakati wa sherehe hiyo.

"Ninashukuru kwa upendo waliouonyesha kwangu japokuwa hii ni sherehe ndogo kwa ajili ya siku hii maalumu kwangu. Sherehe kubwa zaidi inakuja baada ya hapa," alithibitisha.

Ukwa alizaliwa Agosti 1982 katika kijiji cha Mbaitoli kilichoko Jimbo la Imo na amejipatia sifa na umaarufu kutokana na kucheza filamu nyingi akiwa na Aki.

No comments:

Post a Comment