KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 3, 2014

YANGA YAITOA NISHAI MBEYA CITY



YANGA jana ilivuna pointi zote tatu kutoka kwa Mbeya City baada ya kuichapa bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Pamoja na ushindi huo, Yanga imebaki nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 35 baada ya kucheza mechi 16, ikiwa nyuma ya vinara Azam, wanaoongoza kwa kuwa na pointi 36.

Azam iliendelea kujikita kileleni mwa ligi hiyo baada ya jana kutoa kipigo kikali cha mabao 4-0 kwa Kagera Sugar katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Bao pekee na la ushindi la Yanga lilifungwa na mshambuliaji, Mrisho Ngasa dakika ya 16 baada ya krosi ya David Luhende kuokolewa vibaya na beki mmoja wa Mbeya City na mpira kumkuta mfungaji.

Mbeya City ililazimika kumaliza mchezo huo ikiwa na wachezaji 10 baada ya kiungo Steven Mazanda kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kutoa lugha chafu kwa mwamuzi.

Yanga: Deogratius Munishi ‘Dida’, Mbuyu Twite/Juma Abdul dk63, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Frank Domayo, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbangu/Hamisi Kiiza dk70, Mrisho Ngassa na David Luhende.

Mbeya City: David Burahn, John Kabanda, Hassan Mwasapili, Deogratius Julius, Yussuf Abdallah, Anthony Matogolo, Mwagane Yeya/Saad Kipanga dk75, Steven Mazanda, Paul Nonga/Richard Peter dk63, Peter Mapunda na Deus Kaseke/Joseph Willson dk70.

No comments:

Post a Comment