KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 3, 2014

SIMBA YAPELEKA KIKOSI CHA MAUAJI MOROGORO, KUIVAA MTIBWA J'TANO


TIMU ya Soka ya Simba leo (Februari 3), imeondoka jijini kuelekea mjini Morogoro tayari kwa pambano lake la Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa Sugar litakalofanyika keshokutwa (Februari 5) katika Uwanja wa Jamhruri, Morogoro.

Timu hiyo imeondoka ikiwa na kikosi cha wachezaji 22 na viongozi watano ambapo kitapiga kambi katika hoteli ya Mount Usambara kujiandaa na mchezo huo ambapo kitakuwa ikifanya mazoezi katika Uwanja wa Jamhuri.

Kwa mujibu wa Daktari wa timu hiyo, Yassin Gembe, wachezaji wote wako katika hali nzuri na hakuna majeruhi hata mmoja isipokuwa Nassor Chollo anaeendelea na matibabu ya nyonga ya kushoto pamoja na Gilbert Kaze anayesumbuliwa na goti na kutakiwa kupumzika kwa wiki moja. Pia mchezaji Haruna Shamte aliyekuwa akitumikia adhabu ya kadi tatu za njano atakuwemo katika msafara huo.

Akizungumza mda mfupi kabla ya kuondoka, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Zdravko Logarusic alisema wanaelekea mjini Morogoro wakitarajia kupanda upinzani kutoka kwa Mtibwa kwa vile kila timu inazihitaji pointi ili kuweza kujiimarisha katika msimamo wa ligi hiyo.

Alisema licha ya kutarajia upinzani ana matarajio makubwa ya ushindi katika mchezo huo kwa vile amekiandaa kikosi chake kwa ajili ya kupambana katika kutafuta ushindi.

Wachezaji walioondoka jana ni Ivo Mapunda, Yaw Berko, Abuu Hashim, William Lucian, Issa Rashid, Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Haruna Chanongo, Awadh Juma, Amri Kiemba, Amisi Tambwe, Ramadhani Singano.

Wengine ni Henry Joseph, Abdulhalim Humud, Uhuru Selemani, Said Ndemla, Ramadhani Chombo, Gilbert Kaze, Haruna Shamte, Betram Mwombeki na Ali Badru.

Makocha ni Logarusic, Selemani Matola, Idd Pazi, Meneja Nicco Nyagawa, Daktari Yassin Gembe na Mkuu wa Msafara ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Said Pamba.

No comments:

Post a Comment