KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 28, 2014

TAIFA STARS YAICHAPA MALAWI 1-0


TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars jana iliichapa Malawi bao 1-0katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Taifa Stars iliuanza mchezo huo kwa kasi na kufanya shambulizi la nguvu kwenye lango la Malawi dakika ya tano, lakini shuti la Simon Msuva lilitoka nje ya lango.

Dakika ya 17, Kevin Friday alipewa pasi akiwa nje kidogo ya eneo la hatari, lakini shuti lake lilipaa juu.

Bao la Taifa Stars lilifungwa na Amri Kiemba dakika ya 37 baada ya kuunganisha pasi maridhawa kutoka kwa Shomari Kapombe. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.
Malawi ilifanya mashambulizi ya nguvu kwenye lango la Taifa Stars dakika ya 46, 63 na 80, lakini mara zote mashuti ya Rodrick Gonani yalitoka nje.

No comments:

Post a Comment