KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 13, 2014

SERIKALI YAKIRI HAILINDI KAZI ZA WASANII, YATOA AGIZO KWA COSOTA NA TRA


SERIKALI imekiagiza Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA), kukutana na uongozi wa Mamlaka ya Kodi ya Mapato nchini (TRA), ili kupanga mikakati ya kulinda kazi za wasanii.

Agizo hilo lilitolewa jana bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Mchemba alipokuwa akijibu swali la Martha Mlata (Viti Maalumu-CCM).

Katika swali lake la nyongeza, Martha alitaka kujua serikali imejipanga vipi kulinda kazi za wasanii kwa vile utaratibu wa sasa wa kuweka stempu za TRA umelenga zaidi kukusanya mapato.

Mchemba alikiri kuwa ni kweli kuweka stempu za TRA kwenye kazi za wasanii hakulengi kulinda kazi za wasanii zaidi ya kukusanya mapato ya serikali.

"Hivyo naiagiza COSOTA katika siku tano hizi zijazo, ikutane na TRA ili kupanga njia nzuri za kulinda kazi za wasanii na watuletee mrejesho ili tuone nini la kufanya,"alisema.

No comments:

Post a Comment