KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 28, 2014

MBEYA CITY YAPIGWA 2-1 NA AFC LEOPARDS



Na Mwandishi Wetu

MBEYA City imefungwa mabao 2-1 AFC Leopard ya Kenya katika mchezo wa Kundi B michuano ya Nile Basin uliofanyika kwenye Uwanja Khartoum, Sudan.


Mabao yaliyozamisha Mbeya City katika mchezo wa mashindano hayo mapya ya Baraza la Soka la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) inayofanyika kwa mara ya kwanza mwaka huu yamefungwa na kiungo wa zamani wa Simba SC Mganda Mussa Mudde na Mkenya Paul Were.

Bao la Mbeya City limefungwa na kiungo Deus Kaseke na sasa Leopard inaendelea kuishi kileleni mwa Kundi B kwa kufikisha pointi sita, wakati Mbeya City yenye pointi tatu inabaki nafasi ya pili.

Mchezo huo wa michuano inayoshirikisha mabingwa wa Kombe la FA na washindi wa pili wa Ligi Kuu za nchi wanachama wa CECAFA, ulichezeshwa na refa Khalil Walida aliyesaidiwa na Mohammed Abdallah wote wa Sudan na Bogoreh Farhan wa Djibouti.

Mbeya City; David Burhan, Mwagane Yeya, Hamad Kibopile, Deo Julius, Yohanna Morris, Antohny Matogolo, Deus Kaseke, Steven Mazanda, Paul Nonga, John Kabanda na Themis Felix.

AFC Leopard; Patrick Matasi, Paul Were, Edwin Wafula, Eric Masika, Joseph Shikokoti, Mussa Mudde, Austin Ikenne, Juma Abdallah, Jackson Saleh, Benard Mangoli na Noah Wafula.

No comments:

Post a Comment