KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 13, 2014

MBEYA CITY YAPANGWA KUNDI GUMU KOMBE LA NILE


WAWAKILISHI wa Tanzania Bara katika michuano ya soka ya Kombe la Nile, Mbeya City wamepangwa kundi B pamoja na timu za El Merreikh al Fasher ya Sudan, Elman ya Somalia na AFC Leopards ya Kenya.


Taarifa iliyotolewa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) jana inaonyesha kuwa, michuano hiyo imepangwa kuanza Mei 22 mwaka huu mjini Khartoum, Sudan.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, nchi zote wanachama wa CECAFA zimethibitisha kushiriki katika michuano hiyo, isipokuwa Eritrea. CECAFA inaundwa na nchi wanachama 11.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa kundi A litaundwa na timu za El Merreikh ya Sudan, SC Victoria Universty ya Uganda, Malakia ya Sudan Kusini na Polisi ya Zanzibar.

Kundi C litakuwa na timu za Al Ahli Shandi ya Sudan, Al Masry ya Misri, Defence ya Ethiopia na Dikhil ya Djibouti.

Kundi D litakuwa na timu za Hey Al Arab ya Sudan, Arab Contractors ta Misri, Flambeay de i'Est ya Burundi na Etincelles ya Rwanda.

Michuano hiyo itachezwa katika vituo vya Khartoum, Shandy na Red Sea (Port Sudan).

Katika mechi za ufunguzi, Victoria Universty itacheza na Malakia mjini Khartoum, El Merreikh itakipiga na Polisi wakati Arab Contractors itavaana na Flambeau mjini Port Sudan.

No comments:

Post a Comment