KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 3, 2014

KAPOMBE AANZA KUFANYA MAZOEZI NA AZAM




Mshambuliaji Shomari Kapombe amejiunga rasmi na klabu ya Azam FC na kufanya nayo
mazoezi ili kujiweka fiti kwa wakati huu, ambao hana timu baada ya kugoma kurejea klabu
yake ya Daraja la Nne Ufaransa, AS Cannes.

Tovuti ya Azam FC imemnkukuu Kapombe akisema kwamba ameamua kuja kufanya
Azam FC kwa sababu kwanza ni jirani na eneo analoishi na pia wana vifaa vyote vya vya
mazoezi vitakavyosaidia kumuweka fiti.

Hata hivyo, Kapombe hakutaka kuzama ndani juu ya mustakabali wake wa baadaye,
akisema; “Nimekuja Azam kufanya mazoezi kujiweka fiti tu, basi,”alisema.

Tayari kuna habari kwamba, Kapombe anataka kucheza klabu ya Tanzania ambayo
itashiriki michuano ya Afrika mwakani.

Kiungo huyo anayeweza kucheza nafasi za ulinzi pia, anamaliza Mkataba wake Simba
SC mwezi huu, lakini alikwishaingia Mkataba wa miaka minne na AS Cannes ya
Ufaransa mwaka jana.

Na Simba SC imekubaliana na klabu ya Daraja la Nne Ufaransa, kuununua Mkataba wa
mchezaji huyo arejee kufanya kazi Msimbazi baada ya kushindwa kuendelea kucheza
Ulaya.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe alizungumza na
AS Cannes mwezi uliopita na kufikia makubaliano ya kuuziana Mkataba huo, ili
Kapombe arejee Msikmbazi.

Poppe alisema kwamba Simba SC imekubali kuilipa Cannes kiasi cha Euro 33, 000
ambazo sawa na Sh. Milioni 66 ili kurejeshewa mchezaji wake huyo.

Kapombe alitolewa bure kwenda AS Cannes katikati ya mwaka jana akiwa bado ana
Mkataba na klabu hiyo ya Msimbazi, unaomalizika Aprili mwaka huu.

Baada ya kuwa Ufaransa kwa zaidi ya miezi mitatu, Kapombe alirejea nchini Novemba
mwaka jana kwa ruhusa maalum ya kuja kuichezea timu ya taifa katika mchezo wa
kirafiki dhidi ya Zimbabwe.

Baada ya mchezo huo, mchezaji huyo akaamua kubaki moja kwa moja nyumbani akidai
halipwi mishahara.

IMETOLEWA KUTOKA BLOGU YA BIN ZUBEIRY

No comments:

Post a Comment