KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 27, 2014

TISA WAONGEZWA STARS

KOCHA mpya wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, Mart Nooij ameongeza wachezaji
tisa katika kikosi hicho kinachojiandaa kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi (The
Flames).

Timu hizo mbili zinatarajiwa kumenyana Mei 4 mwaka huu katika mechi ya kirafiki ya
kimataifa itakayochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Wachezaji walioongezwa ni Edward Charles Manyama (JKT Ruvu), Elias Maguli (Ruvu
Shooting), Hassan Dilunga (Yanga), Hussein Javu (Yanga), John Bocco (Azam), Kelvin
Friday (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe
(AC Cannes, Ufaransa).

Beki Kelvin Yondani wa Yanga, ambaye aliitwa awali, ameondolewa katika kikosi hicho
kwa vile ameshindwa kuripoti kambini.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Pemium Lager, inaingia kambini leo (Aprili
28 mwaka huu) jijini Mbeya kujiandaa kwa mechi hiyo dhidi ya Malawi.

No comments:

Post a Comment