KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 27, 2014

NGORONGORO YAITOA KENYA KWA MATUTA


TIMU ya soka ya Taifa ya vijana wa chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro

Heroes imeitoa Kenya katika raundi ya kwanza ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za
Afrika.

Ngorongoro imesonga mbele katika michuano hiyo baada ya kuishinda Kenya kwa penalti 4-3, kufuatia timu hizo mbili kushindwa kufungana katika mechi zote mbili za nyumbani na ugenini.

Kwa matokeo hayo, Ngorongoro inayofundishwa na kocha mzalendo John Simkoko
sasa itamenyana na Nigeria katika hatua inayofuata.

Penalti za Tanzania zilikwamishwa wavuni na Mohammed Hussein, Kevin Friday,
Mange Chagula na Iddi Suleiman wakati Mudathir Yahya alikosa.

Penalti za Kenya zilifungwa na Geoffrey Shiveka, Timonah Wanyonyi na Victor Ndinya,
wakati Evans Makari na Harison Nzivo walipoteza.

Hakuna kipa aliyeokoa penalti bali wapigaji walikosa kwa kupiga nje.

Mechi hiyo ilikuwa kali na ya ushindani na makipa wa timu zote mbili, Aishi Manula wa
Tanzania na Farouk Shikhalo wa Kenya aliyeanza kabla ya kumpisha Boniface Barasa
dakika ya 88 walifanya kazi nzuri ya kuokoa michomo ya hatari.

No comments:

Post a Comment