KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 3, 2014

YANGA YAKANA KUWATIMUA KASEJA, CHUJI NA YONDANI



Young Africans itashuka dimbani siku ya jumapili kucheza na JKT Ruvu katika muendelezo wa michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara mzunguko wa pili raundi ya 23 mchezo utakaofanyika katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.


Ligi Kuu ya Vodacom inaelekea ukingoni na sasa kila timu ikijitahid kufanya vizuri ili kuweza kujiweka katika mazingira mazuri aidha ya kubakia Ligi Kuu, kupata Ubingwa au kujinusuru kutoshuka daraja.

Young Africans yenye pointi 46 imebakisha michezo minne ambapo ikiweza kushinda yote itafikisha pointi 58 ambazo zinaweza kupitwa na vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Azam FC peke kama itashinda michezo yake yote miatatu iliyosalia.

Baada ya kupoteza mchezo wake dhidi ya Mgambo JKT mwishoni mwa wiki jijini Tanga, Kikosi cha mhoalanzi Hans Van der Pluijm kimeingia kambini jana jioni katika Hoteli ya Kiromo huku kikiendelea kufanya mazoezi katika Uwanja wa Boko Beach Veterani.

Mlinda mlango Deoragtias Munish "Dida" aliyekua majeruhi kwa takribani wiki mbili kwa sasa ameshapona majeraha aliyokuanayo na ameungana na wenzake kambini tayari kwa maandalizi ya mchezo huo wa siku ya jumapili.

Katika mchezo wa awali wa mzunguko wa kwanza timu hizi zilipokutana, Young Africans iliibuka na ushindi wa mabao 4-0

Aidha taarifa zinazosambazwa na baadhi ya vyombo vya kawamba wachezaji Athuman Idd, Kelvin Yondani na Juma Kaseja wamesimamishwa kutokana na timu kufungwa mchezo dhidi ya Mgambo JKT hazina ukweli, wachezaji hao hawajafukuzwa na wapo wanaendelea na mazoezi pamoja na wenzao.

Tunaomba vyombo vya habari kuwa wanatoa taarifa za ukweli na sio kupotosha jamii na mwisho wa siku kuwapa usumbufu viongozi kufanya kazi ya kukanusha.

No comments:

Post a Comment