KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 3, 2014

VYAMA KUMI VYA MIKOA VYATUMA WAWAKILISHI WAKE RCL


Vyama kumi vya mpira wa miguu vya mikoa vimewasilisha majina ya mabingwa wao
watakaoshiriki Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL).

Mabingwa hao ni Arusha (AFC), Kilimanjaro (Panone FC), Lindi (Kariakoo SC),
Manyara (Tanzanite SC), Mara (JKT Rwamukoma), Morogoro (Volcano FC), Mtwara
(Pachoto Shooting Stars), Pwani (Kiluvya United), Shinyanga (Bulyanhulu FC), Singida
(Singida United) na Tanga (African Sports).

Mikoa ambayo haijawasilisha mabingwa wake ni Dar es Salaam, Dodoma, Geita, Iringa,
Kagera, Katavi, Kigoma, Mbeya, Morogoro, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Simiyu na
Tabora wakati mikoa ya Dodoma na Mwanza imeomba kuongezewa muda kutokana na
sababu mbalimbali.

Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliagiza kuwa
mikoa yote iwe imemaliza ligi na kuwasilisha jina la bingwa wake Machi 30 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment