KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, April 27, 2014

NGORONGORO HEROES KURUDIANA NA KENYA LEO


TIMU ya soka ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes leo itamenyana na vijana wenzaao wa Kenya katika mechi ya marudiano Raundi ya Kwanza kuwania tiketi ya fainali za Afrika mwakani nchini Senegal.


Mechi hiyo itakayochezewa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia Saa 10:00 jioni ndiyo itakayoamua timu itakayocheza raundi inayofuata katika michuano hiyo dhidi ya Nigeria.

Ngorongoro Heroes inayofundishwa na John Simkoko ilitoka suluhu na Kenya katika mechi ya kwanza iliyochezwa Machakos, Kenya wiki tatu zilizopita, na imekuwa kambini jijini Dar es Salaam kwa wiki mbili kujiwinda kwa mechi hiyo.

Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 2,000 na sh. 5,000 ambapo Kenya iliyowasili nchini jana (Aprili 25 mwaka huu) usiku imefanya mazoezi yake ya mwisho jana (Aprili 26 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa.

Mechi hiyo itachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi wakiongozwa na Pacifique Ndabihawenimana wakati Kamishna ni Tarig Atta Salih kutoka Sudan. Kila la heri Ngorongoro Heroes.

No comments:

Post a Comment