KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 27, 2010

Genevieve aendelea kuchemsha China

SANYA, China
MATUMAINI ya mrembo wa Tanzania, Genevieve Emmanuel kufanya vizuri katika shindano la kumsaka mrembo wa dunia mwaka huu, yamezidi kuota mbawa baada ya kuvurunda katika kinyang’anyiro cha kuwania mataji ya michezo na mitindo ya mavazi.
Katika kinyang’anyiro hicho, kilichowashirikisha warembo wote 119 wanaoshiriki kwenye shindano hilo, mrembo Lori Moore kutoka Ireland Kaskazini aliibuka mshindi wa taji la michezo wakati mrembo Mariann Birkedal kutoka Norway alitwaa taji la mitindo ya mavazi.
Mashindano ya kuwania mataji hayo pamoja na lile la vazi la ufukweni, hufanyika kabla ya fainali ya shindano hilo. Tayari Genevieve ameshachemsha katika taji la ufukweni, ambalo lilinyakuliwa na Yara Santiago kutoka Puerto Rico.
Washindi wa mataji hayo, wamefuzu moja kwa moja kuingia kwenye fainali ya shindano hilo, ambayo imepangwa kufanyika Oktoba 30 mwaka huu mjini Sanya.
Shindano la kuwania taji la michezo ndilo lililokuwa na mvuto wa aina yake kutokana na washiriki wote kuonyesha vipaji vyao katika michezo mbalimbali. Shindano hilo lilifanyika kwenye ufukwe wa hoteli ya Sheraton.
Mrembo Lori alishinda taji hilo baada ya kufanya vizuri na kutia fora katika michezo ya kuruka juu, mbio fupi na kuogelea. Alama alizozipata katika michezo hiyo ndizo zilizomwezesha kuibuka mshindi.
“Siwezi kuamini. Nimefuzu kuingia fainali,”alisema Lori, ambaye alizawadiwa medali.
Mshindi wa pili wa taji hilo alikuwa Marina Georgievo kutoka Slovakia wakati nafasi ya tatu ilinyakuliwa na Mariann wa Norway. Wote wawili pia walizawadiwa medali.
Katika kinyang’anyiro cha kuwania taji la mitindo ya mavazi, Mariann kutoka Norway aliibuka mshindi akifuatiwa na mrembo Irina Sharipova kutoka Russia na Alexandria Mills kutoka Marekani.
Katika kuwania taji hilo, washiriki walichuana kwa mavazi mbalimbali yaliyobuniwa na wabunifu maarufu wa mavazi wa China na kuwapa wakati mgumu majaji katika kuamua mshindi.
“Kwa kweli siwezi kuamini kwamba nimewashinda wasichana wengi na kuibuka mshindi wa taji hili,”alisema Mariann. “Ni heshima kubwa kwangu na bila shaka, nimefurahia kuingia fainali.”

No comments:

Post a Comment