KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 30, 2017

TAIFA STARS YAIPIGA BURUNDI 2-0


MSHAMBULIAJI kinda wa Kagera Sugar, Mbaraka Yussuf jana aliibuka shujaa wa timu ya Taifa, Taifa Stars baada ya kuifungia bao la pili na la ushindi dhidi ya Burundi.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yussuf, ambaye apelekwa Kagera Sugar kwa mkopo akitokea Simba, alifunga bao hilo dakika ya 77.

Mpira uliozaa bao hilo ulianzia kwa Simon Msuva katikati ya uwanja, aliyemsogezea Yussuf, ambaye alikimbia nao hadi nje kidogo ya eneo la hatari la Burundi, akafumua shuti likagonga mwamba wa goli, mpira uliporudi akauwahi na kuutumbukiza kimiani.

Mechi hiyo ilikuwa ya kwanza kwa Yussuf tangu alipoitwa kwenye kikosi hicho kwa mara ya kwanza na Kocha Mkuu mpya, Salum Mayanga, ambaye sasa ameweka rekodi ya kushinda mechi mbili.

Taifa Stars ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 22 lililofungwa na Msuva kwa shuti kali baada ya kuuwahi mpira uliopigwa kwa kichwa na Ibrahim Ajib, aliyepewa pasi ya juu na Mohamed Hussein. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.

Burundi ilikianza kipindi cha pili kwa kasi na kufanikiwa kusawazisha dakika ya 53 kwa bao lililofungwa na mshambuliaji wa Simba, Laudin Mavugo, kutokana na uzembe wa beki wa kati wa Taifa Stars, Abdi Banda.

No comments:

Post a Comment