KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 9, 2017

KUZIONA YANGA, ZANACO BUKU TATU



KIINGILIO cha chini katika mchezo wa kwanza hatua ya 32 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya wenyeji, Yanga SC na Zanaco ya Zambia Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa Sh. 3,000.
Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa ametaja viingilio vya mchezo huo juzi wakati akizungumza na wanahabari kwamba, VIP A itakuwa Sh. 20,000 na VIP B na C kote mashabiki watakaa kwa Sh. 15,000.
Mchezo huo utanyeshwa moja kwa na Televisheni ya Azam, jambo ambalo ni faraja kwa mashabiki wa timu hiyo ambao hawataweza kwenda uwanjani, hususan wa nje ya Dar es Salaam.

Yanga ilifuzu hatua ya 32 bora ya michuano hiyo, baada ya kuitoa Ngaya Club de Mde ya Comoro kwa jumla ya mabao matano kwa mawili, ikishinda matano kwa moja mjini Moroni na kulazimishwa sare ya bao moja kwa moja Dar es Salaam, wakati Zanaco iliitoa APR ya Rwanda kwa bao moja bila, ililoshinda Kigali kufuatia sare ya bila bila mjini Lusaka.

No comments:

Post a Comment