KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 20, 2017

MAVUGO AIPELEKA SIMBA NUSU FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO


MSHAMBULIAJI Laudit Mavugo jana aliivusha Simba katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho, baada ya kuifungia bao la pekee ilipoichapa Madini FC bao 1-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha, Madini ilionyesha kiwango safi cha soka na kuwapa wakati mgumu wachezaji wa Simba.

Mavugo, mchezaji wa kimataifa wa Burundi, alifunga bao hilo la pekee dakika ya 55 kwa kichwa, baada ya kupigwa krosi kutoka pembeni ya uwanja.

Simba sasa inaungana na Mbao FC ya Mwanza, iliyowatoa wenyeji, Kagera Sugar kwa mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Mechi nyingine mbili mbili za robo fainali kati ya Azam FC na Ndanda FC na Yanga SC na Prisons zitapangiwa tarehe nyingine.

No comments:

Post a Comment