KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, March 14, 2017

MAYANGA ATANGAZA KIKOSI CHA WACHEZAJI 26 WA TAIFA STARS



KOCHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Salum Mayanga ameita wachezaji 26 kwa ajili ya maandalizi maandalizi ya michezo ya kufuzu michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) na Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).

Katika kikosi hicho, Mayanga hajawajumuisha mabeki wa Yanga, Juma Abdul, Kevin Yondan, Mwinyi Hajji na wa Azam, Aggrey Morris na David Mwantika.

Kuhusu Mngwali na wachezaji wengine wa Zanzibar, Mayanga amesema hajawaita kwa sababu anasubiri maamuzi ya kikao cha Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Machi 16 kuhusu kuipa uanachama nchi hiyo.

"Kama Zanziabr itapewa uanachama CAF, ina maana hatutaendelea kuchanganyika na Zanzibar, lakini kama ikikwama, basi nitawarudisha wachezaji wa Zanzibar, nimeacha nafasi nne kwa ajili hiyo," amesema.

Mayanga aliyetaja kikosi hicho juzi katika Mkutano na Waandishi wa Habari ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ilala, Dar es Salaam - amewachukua washambuliaji chipukizi, Mbaraka Yussuf wa Kagera Sugar na Abdulrahman Juma wa Ruvu Shooting.

Kwa ujumla kikosi alichoteua Mayanga kinaundwa na makipa; Aishi Manula (Azam), Deogratius Munishi ‘Dida’ (Yanga) na Said Mohammed (Mtibwa Sugar).

Mabeki; Shomary Kapombe (Azam), Hassan Kessy (Yanga), Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ (Simba), Gardiel Michael (Azam), Andrew Vincent (Yanga), Salim Mbonde (Mtibwa Sugar), Abdi Banda (Simba) na Erasto Nyoni (Azam FC).

Viungo ni Himid Mao (Azam), Jonas Mkude (Simba), Salum Abubakar ‘Sure Boy’ (Azam), Said Ndemla (Simba), Frank Domayo (Azam), Muzamil Yassin (Simba), Simon Msuva (Yanga), Shiza Kichuya (Simba), Farid Mussa (DC Tennerife) na Hassan Kabunda (Mwadui FC).

Washambuliaji ni Mbwana Samatta (KRC Genk, Ubelgiji), Thomas Ulimwengu (AFC Eskilstuna, Sweden), Ibrahim Hajib (Simba), Mbarak Yussuf (Kagera Sugar) na Abdulrahman Mussa (Ruvu Shooting).

No comments:

Post a Comment