KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, March 14, 2017

RAIS MAGUFULI APIGA SIMU CLOUDS, AZUNGUMZA NA DIAMOND, AAHIDI KUKUTANA NA WASANII


RAIS Dk. John Magufuli ameahidi kukutana na wasanii wa fani mbalimbali nchini kwa lengo la kuzungumza nao kuhusu maendeleo yao na changamoto zinazowakabili.

Alitoa ahadi hiyo leo, baada ya kupiga simu na kuzungumza na msanii Naseeb Abdul 'Diamond', kupitia kipindi cha Clouds 360, kilichorushwa na kituo cha televisheni cha Clouds.

Rais Magufuli aliamua kupiga simu baada ya kumsikia Diamond akimuomba asaidie sanaa ya muziki kama anavyosaidia katika mambo mengine.

”Mimi namuomba Rais Magufuli, kama anavyosaidia mengine kwa wepesi, kwenye sanaa uweke mkono wako Baba tunakutegemea,” alisema Diamond.

Baada ya Diamond kuyaomba hayo, Rais Maguli alipiga simu moja kwa moja kwenye kipindi hicho na kusema: “Nimemsikia Diamond na maombi yake nimeyapokea kwa mikono miwili. Nimefurahi kumskia siku ya leo, natafuta siku ambayo tutakaa pamoja. Nasikilizaga nyimbo zako hata wale wanaoigiza nawapenda sana na SHILAWADU,” alisema Rais Magufuli.

Aliongeza: “Hongera sana Diamond hongera sana kuwa na watoto, wakati wa kampeni ulikuwa na mtoto mmoja sasa una wawili.“

NUKUU ZA DIAMOND KATIKA MAHOJIANO HAYO:

Watu wanashangaa mimi kutangaza vivutio vya Afrika Kusini, sio kwamba nimekosa uzalendo, wameniona kupitia sanaa.

Tumeanzisha mtandao wetu wa kuuza na kusambaza nyimbo za wasanii online, tumeongea na mashabiki watuunge mkono

Nilishawahi kwenda TANAPA kuomba niwe balozi wa utalii nitangaze nchi yangu, lakini walitaka nijitolee bure tu

Msanii akihusishwa kwenye sakata la dawa za kulevya ni kuharibu brand, serikali itumie busara kuzilinda na kesi

Makonda ni mlezi wa WCB, kila mwanadamu ana mapungufu yake, tuangalie pia mazuri, ameonesha uthubutu kwenye kazi.

Tangu mwezi wa saba mpaka sasa sijapokea mauzo yangu, nimeyasusa, kinachofuata itakuwa ni hatua za kimahakama.

Mimi ni kielelezo ndani na nje ya nchi, watu wengi wameifahamu Tanzania kupitia sanaa yetu, lazima tujijenge.

Kipindi tunamuaga Rais Kikwete, nilipata nafasi ya kuzungumza na Rais Magufuli, nilimuomba tupate ukumbi wa kisasa

Watu walizungumza vibaya mimi kupewa benderĂ , ilisaidia sana kulitangaza taifa letu, nilimuomba Nape samahani

Tulilipa kodi ya TRA shilingi milioni 35, ni uthubutu, tunaweza kulipa kodi nyingi, serikali inabidi itulinde kwenye sanaa.

Nilikutana na Alikiba, Nairobi, tukazungumza, maneno yanasemwa na watu wa katikati, baadhi ya media zinachochea tu

Hili suala la Serengeti Boys ni jukumu letu kulibeba kama Taifa, tuunganishe nguvu ushindi wetu ushindi wao.

Naomba serikali iwasaidie vijana wa vibanda vya chipsi pamoja na bodaboda ishu ya muda wa saa sita wapewe ulinzi

Wakati huo huo, mwimbaji wa BongoFleva, Vanessa Mdee, ameachiwa na polisi kwa dhamana, baada ya kusota rumande kwa siku tano.

Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Simon Sirro, amethibitisha kwamba Vanessa, ameachiwa kwa dhamana.

“Ndio, tumempa dhamana wakati tunaendelea na uchunguzi, amepewa ataripoti kesho,” alisema.

No comments:

Post a Comment