KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 16, 2017

BREAKING NEWSSSSSS. ZANZIBAR YAPATA UANACHAMA CAF


HATIMAYE Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), limekubali kuipatia Zanzibar, uanachama wa shirikisho hilo.

Uamuzi huo umefikiwa leo, wakati wa mkutano mkuu wa CAF, uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Zanzibar sasa inakuwa mwanachama wa 55 wa CAF na itaanza kushiriki katika michuano ya Mataifa ya Afrika na ile ya vijana wa umri mbalimbali.

Aidha, Zanzibar sasa itaanza kupata mgawo wa CAF kwa nchi wanachama wa shirikisho hilo kwa ajili ya shughuli mbalimbali, ikiwemo kuendeleza soka.

Kabla ya kupitishwa kwa uamuzi huo, Zanzibar ilikuwa ikiruhusiwa kushiriki katika mashindano ya klabu bingwa Afrika na Kombe la Shirikisho.


No comments:

Post a Comment