KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, March 5, 2017

YANGA YAFUFUA MATUMAINI YA UBINGWA


YANGA jana ilirejesha matumaini ya kutwaa tena taji la ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Ruvu Shooting mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo uliiwezesha Yanga ifikishe pointi 52 baada ya kucheza mechi 23, ikiwa nyuma ya vinara Simba wenye pointi 54 kutokana na idadi hiyo ya michezo.

Yanga ilijikuta ikimaliza mchezo huo ikiwa pungufu baada ya mchezaji Obrey Chirwa kutolewa nje kwa kadi nyekundu, ambayo ilizua utata kutokana na mazingira ya kutolewa kwake.

Awali, Chirwa alionyeshwa kadi ya njano dakika ya 44 baada ya kuifungia Yanga bao safi ambalo lingekuwa la pili kwa kichwa akimalizia krosi ya beki wa kulia, Hassan Kessy, lakini refa Ahmada Simba wa Kagera akalikataa na kumuonyesha kadi ya njano.

Na Mzambia huyo akaonyeshwa kadi ya pili njano dakika ya 45 baada ya kuudunda mpira chini na kutolewa kwa kadi nyekundu.

Iliwachukua Yanga dakika 47 kuhesabu bao la kwanza kupitia kwa Amissi Tambwe kabla ya Emmanuel Martin kuongeza la pili dakika za nyongeza.

No comments:

Post a Comment