KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 6, 2017

YANGA YABANWA MBAVU NA MTIBWA, MSUVA AKOSA PENALTI


MABINGWA watetezi Yanga jana walibanwa mbavu na Mtibwa Sugar baada ya kulazimishwa kutoka nayo suluhu katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Iwapo Yanga ingeshinda pambano hilo, ingeweza kuiengua Simba kileleni mwa ligi kwa kuongoza kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa kwani zote zingekuwa na pointi 55 baada ya kucheza mechi 24.

Lakini kutokana na sare hiyo, Yanga imeendelea kushika nafasi ya pili ikiwa na pointi 53 huku Simba ikiendelea kuongoza kwa kuwa na pointi 55.

Yanga itabidi ijilaumu kwa kushindwa kutoka uwanjani na ushindi kwani ilipata penalti dakika ya 35, lakini shuti la Simon Msuva lilitoka nje ya lango.

No comments:

Post a Comment