KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 20, 2017

AZAM YATUPWA NJE KOMBE LA SHIRIKISHO


WAWAKILISHI wengine wa Tanzania katika michuano ya Afrika, Azam jana walitupwa nje katika michuano ya Kombe la Shirikisho, baada ya kuchapwa mabao 3-0 na Mbabane Swallows.

Kipigo hicho kimeifanya Azam itolewe nje ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 3-1, kufuatia kushinda mechi ya awali mjini Dar es Salaam kwa bao 1-0.

Kabla ya pambano hilo, kulikuwepo na vitendo visivyo vya kiungwana, ambavyo polisi na mashabiki wa Swaziland waliwafanyia viongozi na wachezaji wa Azam.

Pengine kitendo kibaya zaidi kilikuwa wakati wachezaji wa Azam waliposhindwa kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kwa madai kuwa wenyeji walivipulizia dawa kali ya sumu.

No comments:

Post a Comment