KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 22, 2015

TWIGA STARS KUJIPIMA KWA WAKENYA KESHO



Timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) inatarajiwa kushuka dimbani siku ya jumapili kucheza dhidi ya timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Starlets) katika uwanja wa Amani kisiwani Zanzibar ukiwa ni mchezo wa kirafiki.

Kocha mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage amesema anaendelea vizuri na maandalizi, vijana wake wote wapo katika hali nzuri kuelekea katika mchezo huo wa kirafiki kabla ya safari ya kuelekea nchin Congo-Brazzavile.

Twiga Stars inatumia mchezo huo wa kirafiki kama sehemu ya maandalizi ya fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) zinazofanyika kuanzia Septemba 4-19 nchini Congo-Brazzavile

Timu ya Taifa ya Wanawake ya Kenya (Harambee Starlets) tayari imewasili kisiwani Zanzibar ikiwa na kikosi cha wachezaji 17 pamoja na viongozi 9 tayari kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya Twiga Stars siku ya jumapili.

Mchezo huo wa kirafiki unatarajiwa kuanza majira ya saa 10 kamili jioni katika Uwanja wa Amani kisiwani Zanzibar, ambapo viingilio vya mchezo huo itakua ni shilingi elfu mbili kwa jukwaa kuu, na shilingi elfu moja kwa mzunguko.

No comments:

Post a Comment