KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, August 5, 2015

DIRISHA LA USAJILI KUFUNGWA KESHO



Dirisha la Usajili kwa wachezaji wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), Ligi Daraja la kwanza (FDL), na Ligi Daraja la Pili (SDL) linatarajiwa kufungwa kesho Alhamis saa sita usiku.

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), linavikumbusha vilabu vyote vinavyoshirki msimu mpya wa 2015/2015 kuhakikisha vinakamilisha usajili wa wachezaji wao kabla ya dirisha la usajili kufungwa kesho.

Kipindi cha dirisha la usajili kwa timu za Ligi Kuu, Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kilifunguliwa Juni 15, 2015 na kitamalizika kesho kwa awamu ya kwanza ya usajili.


No comments:

Post a Comment