KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 29, 2015

NYOTA WATANO U15 WAENDA ORLANDO PIRATES KUJARIBIWA



Wachezaji watano kutoka katika kikosi cha vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U-15) wanaondoka leo jijini Dar es salaam kuelekea nchini Afrika Kusini katika klabu ya Orlando Pirates kwa ajili ya kufanya majaribio.

Vijana hao wanakwenda katika klabu ya vijana ya Orlando Pirates kufanya majaribo ambapo makocha wa vijana wa klabu hiyo watapata nafasi ya kuwatazama katika mazoezi na michezo ya kirafiki.

Nafasi hiyo imepatikana kufuatia mazungumzo ya Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Rais wa klabu hiyo Irvin Khoza kuomba vijana hao kupata nafasi ya kufanya majaribio katika klabu hiyo na endapo watafuzu, watajiunga na timu ya vijana ya Orlando Pirates.

Msafara huo wa wachezaji utaongozwa na Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi ambaye atakua na vijana hao katika kipindi chote cha majaribio nchini Afrika Kusini.

Wachezaji hao ni Asaad Ali Juma (Zanzibar), Maziku Aman (Dodoma), Issa Abdi (Dodoma), Kelvin Deogratias (Geita) na Athumani Maulid (Kigoma).

Shirkisho la Mpira wa Miguu nchini linawatakiwa kila la kheri vijana hao katika majaribio yao huko nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment