KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 22, 2015

DRFA YAPUUZA AGIZO LA TFF


Kamati ya uchaguzi ya chama cha soka mkoa wa Dar e salaam DRFA,imeshindwa kutekeleza agizo la lililotolewa na mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF la kusimamisha mchakato wa uchaguzi wa chama cha soka wilaya ya temeke TEFA uliopangwa kufanyika jumapili agosti 23/2015.

Baada ya kupitia kwa umakini kanuni za uchaguzi za TFF za mwaka 2013 ibara ya 6, na kujiridhisha kuwa hakuna kipengele chochote kinachoruhusu kamati ya uchaguzi ya TFF kuingilia kati mchakato wa uchaguzi wa TEFA,Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya DRFA,Rashid Saadallah,(mwanasheria ),amemuandikia barua mwenyekiti wa uchaguzi wa TFF,Aloyce Komba kumjulisha hilo na kumueleza kuwa mchakato huo sasa utaendelea kama ulivyopangwa kufanyika jumapili agosti 23/2015.

Mwenyekiti huyo wa uchaguzi DRFA,amesema mpaka sasa taratibu na maandalizi yote kuelekea uchaguzi huo wa jumapili yamekamilika ikiwemo usikilizwaji wa rufaa mbalimbali na kuzitolea uamuzi,hivyo  kitendo cha kuingilia kati mchakato huo ni kinyume cha utaratibu,kwa kuwa TEFA ni mwanachama wa DRFA na siyo wa TFF.

WASHIRIKI WA KOZI YA UKOCHA LESENI ‘C’WAKUMBUSHWA KULIPIA ADA ZAO.

Washiriki wa kozi ya ukocha kwa ngazi ya leseni ‘C’ iliyoandaliwa na shirikisho la soka barani afrika CAF pamoja na chama cha soka mkoa wa Dar es salaam DRFA,ambayo inayotarajiwa kuanza tarehe 28/ 08/ 2015,wanakumbushwa kulipia ada zao  za ushiriki kwenye kozi hiyo,itakayofanyika katika ukumbi wa ofisi za TFF zilizopo uwanja wa karume jijini Dar es salaam.

Kiasi cha ADA kilichopangwa kulipwa ni shilingi laki mbili na elfu hamsini ( TZS 250,000),ambazo zinatakiwa kulipwa kwenye benki ya Akiba tawi la IIala Branch lililopo katika jengo la Machinga Complex,na ilipwe kwa  ( Account number 010100548227)

Kozi hiyo imepangwa kufanyika katika madarasa mawili yatakayokuwa na wanafunzi  30 kila darasa

No comments:

Post a Comment